Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme (kulia) akizungumza na mdau wa Nishati Safi ya Kupikia katika mabanda yaliyowekwa nje ya ukumbi wa mkutano ambao Mdahalo wa Nishati Safi ya Kupikia ulikuwa ukifanyika Unguja, Kizimkazi Agosti 23, 2024
Aidha Naibu katibu Mkuu huyo amesema binafsi amefurahishwa na jamii kuendelea kuelimika juu ya umuhimu wa matumizi ya Nishati safi ya kupikia ikiwepo matumizi ya gesi kuongezeka majumbani jambo ambalo linapunguza uharibifu wa Mazingira kwa kiasi kikubwa.
“…Ni dhamira na lengo kuu la Mhe.Rais Samia kuona wananchi wanatumia nishati zisizochaafua mazingira kwani ni moja ya kipimo cha kuwa na jamii iliuostaarabika na yenye mazingira salama ambapo sisi kama wizara ni lazima tukahakikishe tunasimamia na kuunga mkono dhamira hii njema ya Mhe.Rais Wetu”amesema Bi Mndeme