
Mwigizaji wa filamu za Kibongo, Irene Pancras Uwoya, amelowa mvua ya
matusi baada ya kumfananisha mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’
na aliyekuwa mwanamuziki mkubwa duniani, marehemu Michael Jackson.
Wikiendi iliyopita, Uwoya aliandika kwenye ukurasa wake katika mtandao
wa Instagram kuwa msanii huyo anayefanya vizuri katika Bongo Fleva ndiye
staa atakayemrithi mkali huyo wa Pop, maandishi ambayo yalizua matusi
hayo ya nguoni.
Baadhi ya mashabiki wa mastaa hao walitoa maoni kuwa
jambo hilo ni sawa na kufananisha vitu ambavyo havina uwiano hasa
ukizingatia Michael Jackson alishafariki dunia Juni 25, 2009.
“Sasa
hiyo ni akili gani ya ki…(tusi) kumfananisha mtu aliyeko hai na
marehemu?” alihoji Mishish, mmoja wa mashabiki wa Uwoya katika mtandao
wa Facebook baada ya ishu hiyo kuwa gumzo mitandaoni.
“Kweli wewe
Irene (Uwoya) ni …(tusi) au kwa sababu Diamond amesha…(tusi) ndiyo maana
unamsifia kiasi hicho,” aliandika shabiki mwingine kwenye Twitter na
kupisha wengine kuendelea kumporomoshea Uwoya matusi ya nguoni.