Hatimaye Mama Mercy Anna Mengi Azikwa Moshi

Special Correspondent6 years ago6 Views

Hatimaye Mama Mercy Anna Mengi Azikwa Moshi

Mwili wa mmoja wa waanzilishi wa makampuni ya IPP Mama Mercy Anna Mengi, umezikwa leo eneo la Wari Machame Moshi, Mkoani Kilimanjaro ambapo mamia ya watu kutoka mikoa mbalimbali ikiwemo Kilimanjaro na Dar es salaam wameshiriki mazishi hayo.

Awali mwili wa Mama Mercy Anna Mengi uliagwa katika Kanisa la KKKT usharika wa Moshi mjini, ibada ambayo iliongozwa na Askofu Dkt Fredrick Shoo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kisiasa na watu maarufu.


Katika ibada hiyo pia Makamu wa Rais, Samia Suluhu pia alishiriki ambaye aliambatana na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Suleiman Jaffo pamoja na viongozi wengine wa kisiasa akiwemo Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe.


Mama Mercy Anna Mengi aliaga dunia tarehe 31 Oktoba, 2018 katika hospitali ya Mediclinic Morningside, Johannesburg Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu.


Mwili wa Marehemu Mama Mercy Anna Mengi uliwasili Jijini Dar es Salaam tarehe 7 Novemba, 2018. Na Ibada ya kumuaga ilifanyika katika Kanisa la Azania Front Alhamis ya tarehe 8 Novemba 2018 jijini Dar es salaam.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.