BABA mzazi wa Meneja wa
Nasibu Abdul ‘Diamond’, Babu Tale, amezikwa juzi Jumanne kijijini kwao
Mkuyuni, mjini Morogoro lakini miongoni mwa mambo ya kushangaza ni
kitendo cha baadhi ya waombolezaji kumsaka mwanamuziki Nasibu bila
mafanikio.
Staa wa Bongo fleva Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Hilo lilijitokeza baada
ya msafara uliotokea Dar kufika eneo hilo ambapo vijana walilizingira
gari lililokuwa na mastaa na kuanza kuuliza juu ya uwepo wa
Diamond.Vijana hao waliotarajia kumuona msanii huyo msibani hapo, hata
waliposikia tetesi kuwa hakuwepo, waliendelea kumsaka kila gari huku
wakimuuliza kila waliyemuona lakini jibu lilikuwa lilelile, hakufika.
Majibu hayo yalionekana
kuwanyong’onyesha vijana hao ambapo baadhi waliamua kuondoka kuonesha
dhahiri kuwa kilichowapeleka pale ni kumuona Diamond na si kuzika.Hata
hivyo, vijana wengine waliamua kujipoza kwa kupiga picha na Madee kisha
kushiriki mazishi hayo mwanzo mwisho.