Aliyekuwa Makamu wa rais wa kampuni ya Acacia na Wenzake Waendelea Kusota Rumande

Special Correspondent6 years ago6 Views

Aliyekuwa makamu wa rais wa kampuni ya Acacia, Deo Mwanyika na wenzake watakula Sikukuu ya Krisimasi na Mwaka Mpya gerezani baada ya upande wa mashtaka kuieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa upelelezi wa kesi yao bado haujakamilika.

Wakili wa Serikali, Simon Wankyo amedai hayo leo Ijumaa Desemba 21, 2018 kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Hakimu Mkazi Mfawidhi, Kelvin Mhina ameahirisha kesi hiyo  hadi Januari 4, 2019.

Mbali na Mwanyika, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni meneja uhusiano wa mgodi wa Bulyanhulu,  Alex Lugendo; mkurugenzi mtendaji wa Pongea, North Mara na Bulyanhuku Assa Mwaipopo; kampuni ya mgodi ya Pangea, North Mara, Exploration na Bulyanhulu.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 39, yakiwemo ya utakatishaji na kukwepa kodi zaidi ya Dola 112 milioni za Marekani.

Washtakiwa hao pia wanakabiliwa na mashtaka matatu ya kula njama, saba ya kughushi, 17 ya utakatishaji wa fedha, kuwasilisha nyaraka za uongo kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), shtaka moja la  kuongoza uhalifu wa kupangwa, mashtaka manane ya kukwepa kodi na moja la kutoa rushwa.

from MPEKUZI http://bit.ly/2EBEFsE

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.