Kylian Mbappé Apiga Chini Fuko la Hela Kutoka Kwa Waarabu Saudi Arabia

2 years ago105 Views

 
Kylian Mbappé hana nia ya kufungua mazungumzo na Al Hilal kwa sasa. Apiga chini mshahara wa Euro Milioni 700 zaidi ya TZS Trilioni 2 kwa mwaka na zaidi ya TZS Bilioni 36.5 kwa wiki.

Amekataa kufanya mazungumzo na klabu hiyo ya Saudi Arabia baada kutenga kitita cha Euro Milioni 300, dau ambalo halijawahi kutokea kwenye historia ya mpira wa miguu, ili kuinasa saini ya mshambuliaji huyo wa Ufaransa anayekipiga kunako klabu ya Paris Saint-Germain.

Mbappe mwenye umri wa miaka 24 amewekwa sokoni na mabingwa hao wa Ufaransa baada ya kukataa kusaini mkataba mpya, huku mkataba wake wa sasa ukitarajiwa kutamatika msimu ujao.

Vyanzo vya karibu na PSG vimeripoti kuwa klabu hiyo imesalia kushawishika kuwa Kylian Mbappé alikubaliana na Real Madrid katika uhamisho wa majira ya joto 2024.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.