ZARI AFUNGUKA MAZITO KUHUSU “WATANZANIA MSIKIE MWISHO AAMUA KUSEMA YOTE NI HERI KABISA”..DAH HIVI NI KWA NINI?IPO HAPA

Admin Updates10 years ago5 Views



Zari Tlale aka The Bosslady amesema upendo anaoupata baada ya kuanzisha
uhusiano na Diamond Platnumz, umemfanya agundue kuwa watanzania
wamemkubali kama mtu wao.

Akiongea na Clouds FM/TV asubuhi hii, Zari amesema tangu ameanza kuja
Tanzania amekuwa akipokea upendo zaidi kutoka kwa watanzania kiasi
ambacho kimemfanya ajisikie kama yupo kwao.

“Siwezi hata kulalamika, watu wa Tanzania ni wakarimu sana ni watu
wazuri sana, kwangu mimi sijapata hata tatizo, siwezi hata kusema kitu
chochote kibaya kuhusu watu wa Tanzania,” alisema.

“Wamenikaribisha kama ni mtu wao na sasa mimi ni wao hivyo ni yote ni heri kabisa,” aliongeza.

Katika hatua nyingine Zari amesema Tanzania itageuka kuwa makazi yake ya
mara kwa mara na mipango iliyopo ni kuanzisha mradi wa kibiashara
nchini lakini baada ya kufanya utafiti na kubaini fursa za uhakika.

“Siwezi tu nikafungua biashara hapa eti kwasababu mimi ni maarufu
nikafungua tu biashara ya kijinga na nikidhani ninaweza nikauza wazo
langu la kijinga kwa watu hapa, wao sio wajinga wanatumia hela zao hivyo
nahitaji kubaini wapi kuna hitaji, kipi naweza kufanya na hapo ndipo
ntaenda na kuwekeza fedha zangu.”

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.