Yanga Waonyeshwa Mwangaza wa Ushindi Mkubwa Rwanda

Admin Updates1 year ago4 Views

KIUNGO wa kimataifa wa Rwanda ambaye amewahi kukipiga ndani ya timu za Simba na Yanga, Haruna Niyonzima, amesema mbali na mapokezi makubwa ambayo kikosi cha Yanga itayapata itakapotua nchini Rwanda, pia anaamini timu hiyo ina uwezo mkubwa wa kuifunga Al Merrikh.

Septemba 16, mwaka huu, Yanga wanatarajiwa kuvaana na Al Merrikhya Sudan, katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa hatua ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika utakaochezwa nchini Rwanda kusaka tiketi ya kufuzu hatua ya makundi.

Kwa vipindi vitatu tofauti, Niyonzima amewahi kuhudumu katika timu za Simba na Yanga, huku akifanikiwa kushinda makombe matano ya Ligi Kuu Bara ndani ya misimu mitatu mfululizo.

Akizungumzia mchezo huo, Niyonzima alisema: “Nafurahi kuona timu yangu ya Yanga inakuja hapa Rwanda kwa ajili ya mchezo wa kimataifa dhidi ya Al Merrikh, napenda kuwaahidi kuwa nitakuwa mstari wa mbele kuongoza mapokezi, lakini pia kuhakikisha Yanga inapata matokeo ya ushindi na kuondoka hapa wakiwa na tabasamu.”

 

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.