Hamida Hassan na Gladnes Mallya
Staa wa filamu za Kibongo, Lungi Maulanga amemshangaa msanii mwenzake
Jacqueline Wolper kwa kutoka kimapenzi na mwanaume wake aitwaye Jimmy.
Sosi wa karibu na mastaa hao alidai kuwa, baada ya hivi karubuni
gazeti ndugu na hili la Risasi Jumamosi kuandika kuwa Wolper amepata
kigogo mpya aitwaye Jimmy, Lungi alishangaa, akajiuliza imekuwaje tena
Wolper aamue kutembea na shemeji yake.
Ili kupata ubuyu uliokamilika, Ijumaa lilimtafuta Lungi
akasema: “Ni kweli Jimmy alikuwa mtu wangu, tukatofautiana kidogo,
alipoenda Sauzi akakutana na Wolper ikadaiwa kuwa walitoka kimapenzi,
nilishangaa kusikia hivyo na nimeamua kuachana na huyo Jimmy mwenyewe.
Wolper alipotafutwa kuzungumzia madai hayo alijitetea kwa kusema,
yeye hajatoka na Jimmy ila walikutana tu Sauzi na kupeana kampani ya
kawaida tu.