Na Juma Nyumayo, Songea
Katibu Tawala wa Wilaya ya Songea Mtela Mwampamba amehimiza kutembelea vivutio vya utalii na kuwekeza wilayani Songea.
DAS Mwampamba Ametoa wito huo akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Songea Kapenjama Ndile kwenye Bonanza la Bank ya CRDB lililofanyika Shule ya Sekondari ya De Paul, Songea.
Bonanza lenye kuhamasisha Watumishi wa CRDB utaratibu wa kufanya mazoezi ya viungo ikiwemo utaratibu wa kupima afya zao kila wakati na kuzingatia lishe Bora.
Mwampamba ametumia Bonanza hilo kuwahimiza na kuwakaribisha Watumishi hao na wengine wanaotoka maeneo mbalimbali nchini kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo Wilaya ya Songea ikiwemo Bustani ya wanyama pori, Ruhila Zoo, Makumbusho ya Taifa ya vita vya Majimaji na ya Dkt.Rashid Mfaume Kawawa na alikumbushia kuwa Songea ni Mji wa Kihistoria.
Amewaomba watumishi wa CRDB na wengine kuwekeza Wilayani Songea kwenye Sekta ya Kilimo kabla ya kusubiri kiinua mgongo baada ya Kustaafu.