WANASAYANSI WATOBOA SIRI YA KUTIBU UKIMWI

Special Correspondent6 years ago4 Views

Mtu mmoja huko Uingereza ambaye alikuwa ni muathirika wa UKIMWI, amekuwa mtu wa pili ulimwenguni kupona ugonjwa huo, baada ya kupandikizwa ujiuji katika mifupa ‘bone marrow’.

Ikiwa ni takriban miaka mitatu imepita tangu awekewe cells za bone marrow za kipekee zenye uwezo wa kuzuia maambukizi ya HIV na kutumia dawa maalum, mtu huyo ameonesha kutokuwa na dalili zozote za kwamba aliwahi kuwa na HIV.

“Hakuna virusi ambavyo tunaweza viona, hatuwezi kuvipata”, amesema Dkt. Ravindra Gupta, ambaye pia ni Profesa na mtaalamu wa masuala ya HIV aliyeongoza timu ya wanasayansi kutoa tiba hiyo ya utafiti.

Kutokana na hilo, Dkt Gupta amesema kwamba kesi hii ni uthibitiso tosha wa dhana kwamba ipo siku wanasayansi wataweza kupata tiba rasmi ya UKIMWI na kumaliza kabisa tatizo hili.

 Lakini haimaanishi kuwa wameshaipata tiba kwa sasa.

Mtu huyo kutoka Uingereza anakuwa wa pili ulimwenguni kupata tiba hiyo, baada ya kijana wa Marekani Timothy Brown, kufanyiwa tiba hiyo hiyo na kupona kabisa, huko nchini Ujerumani mwaka 2007.

Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO), ugonjwa wa UKIMWI tayari umeshaua takriban watu milioni 35 duniani tangu ulipoanza katika miaka ya 1980s, na hadi kufikia mwaka 2017 takriban watu milioni 37 wanaishi na virusi vya ugonjwa huo, huku madaktari wakikesha kutafuta tiba kumaliza kabisa ugonjwa huo hatari.

from MALUNDE 1 BLOG https://ift.tt/2ELXHft
via

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.