WADAU WA HABARI WATAKIWA KUZIDI KUELIMISHA JAMII KUHUSU WATU WENYE UALBINO NCHINI

6 years ago66 Views

Na Hussein Stambuli, Morogoro
Wadau wa tasnia ya habari nchini wameombwa kutumia maarifa yao kuielimisha zaidi jamii juu ya uwepo wa watu wanaoishi na ualbino kwani mpaka sasa bado kumekuwa na changamoto ya unyanyapaa dhidi ya watu hao ikiwemo ushirikishwaji wao katika ajira, kuendelea kuwepo kwa matukio machache yanayohusishwa na utekaji pamoja na kuitwa majina yasiyofaa katika jamii wanazoishi jambo linaloashiria unyanyapaa dhidi yao.
Maombi hayo yamefikishwa na Afisa mlaghibishi kutoka shirika la kimataifa lisilokuwa la kiserikali la kutetea usalama, ustawi na haki za watu wenye ualbino  la ‘Under the same Sun’ Kondo Sefu ambapo amesema bado jamii imebaki katika mkondo usio salama dhidi ya watu hao ikiwemo muendelezo wa matukio machache yanayohusishwa na Imani za kishirikina pamoja na ubaguzi.
“Bado hali haijakaa sawa kumekuwa na matukio ya kufukuliwa kwa mifupa ya watu wenye ualbino kwenye makaburi wanayozikwa, majaribio ya kutekwa katika baadhi ya mikoa hili jambo bado linaonesha changamoto ya kurejesha usawa dhidi ya watu wenye ualbino katika jamii bado inahitajika” alisema Kondo
Awali akifungua mafunzo hayo Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo la under the same sun Berthasia Ladislaus alisema kuwa shirika hilo kwa kushirikina na serikali limeweza kusaidia kupunguza matukio ya mauaji na vitendo vingine vya kikatili dhidi ya watu wenye ualbino.
“katika kipindi cha Januari hadi Mei kumekuwa na matukio mawili tu ya matishio ya utekaji wa watu wenye albino katika maeneo ya Ngorongoro na Kwimba ambapo watu wasiojulikana walitaka kuwadhuru watoto wawili wenye albino hata hivyo majaribio hayo hayakufanikiwa” alisema Berthasia.
Pia shirika la kimataifa lisilokuwa la kiserikali la kutetea usalama, ustawi na haki za watu wenye ualbino  la ‘under the same sun’ limewaomba waandishi wa habari kuwa na matumizi sahihi ya lugha wanaporipoti juu ya kundi hilo hasa kuwaita ‘watu wenye ualbino’ badala ya zeruzeru, albino, watu wenye ulemavu wa ngozi pamoja na kufanya Makala maalum juu ya maisha na changamoto wazozipitia jamii ya watu hao.
 Mkurugenzi Mtendaji wa shirika  la under the same sun Berthasia Ladislaus akifafanua jambo mbele ya wahariri mbalimbali waliojitokeza katika semina elekezi juu ya watu wenye ualbino
Wadau wa shirika la kimataifa lisilokuwa la kiserikali la kutetea usalama, ustawi na haki za watu wenye ualbino  la ‘under the same sun’
Wadau wa tasnia ya habari wakiwa katika picha ya pamoja katika semina elekezi inayohusu namna ya kuripoti habari za watu wenye ualbino kwa wahariri

from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2QEcBZO
via

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.