
Msanii Vanessa Mdee ameshindwa kuvumilia maneno ya shabiki mmoja kwenye account ya Instagram ya Jux na kuamua kumtolea povu juu ya maneno yake ya shombo kwa mpenzi wake wa zamani huyo.
Jux aliweka video akifanya show ya pamoja na Vanessa Mdee na moja ya shabiki wa Jux wa kike alianza kumponda Jux kuwa anajipendekeza kwa Vanessa na kwenda mbali zaidi na kusema Vanessa hana haja na yeye na hana kitu cha kumpa.
Kufuatia ujumbe huo Vanessa Mdee alishindwa kuvumilia na kuja kumjibu binti huyo kwa kumweleza kuwa yeye si msemaji wake na kudai amekuwa akitukana kila siku kwenye page hiyo ya Jux na kusema huenda akawa anamtaka Jux.







