Uongozi wa SIMBA Wawaangukia Wachezaji, Ishu Nzima Imekaa Hivi

Admin Updates1 year ago7 Views

Uongozi wa Simba SC umewataka Wachezaji wa Klabu hiyo kupambana na kutambua uchungu wanaoupata Mashabiki na Wanachama pale mambo yanapokwenda mrama.

Ombi hilo kwa Wachezaji wa Simba SC limewekwa hadharani kufuatia mambo kuwaendea mrama wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Young Africans, uliomalizika kwa Mnyama kupigwa 5-1, Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam Novemba 05.

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC Ahmed Ally amesema wachezaji wanapaswa kutambua hilo na kuhakikisha wanapambana vilivyo katika kila mchezo ili kufanikisha furaha kwa Mashabiki na Wanachama ambao wamekuwa bega kwa bega na timu yao.

“Wachezaji sisi tuna imani nao, tarehe 25 wakaendeleze makubwa. Waamke sasa wakaipiganie Simba. Wanayo kazi kubwa ya kutufutia hizi kejeli kwa wao kufanya vizuri. Tukipata matokeo mazuri watapunguza machungu makubwa tunayopita hivi sasa.”

“Ni muhimu wajue pale hawachezi tu kwa ajili yao bali kwa ajili ya Simba. Sisi tutaenda kutimiza wajibu wa kushangilia, na wao watupe furaha ili turejeshe hali yetu ya kutamba. Tunawambia hivyo kwa niaba ya mgeni rasmi, mashabiki wa Simba.” amesema Ahmed Ally

 

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.