
Mkurugenzi mtendaji (Tigo) Bw. Simon Karikari akimkabidhi mfano wa hundi ya Mil 110/- Ofisa Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Brenda Msangi.Hafla ya makabidhiano yalifanyika katika wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika hospitali ya CCBRT
Kampuni ya mawasiliano ya Tigo leo imetoa msaada wa Sh110 milioni kwa Hospitali ya CCBRT kwa lengo la kusaidia uboreshaji wa huduma za afya hasa kwa wagonjwa wenye matatizo ya mguu kifundo (clubfoot) utakaowanufaisha wagonjwa zaidi ya 400 hapa nchini. Msaada huu unatolewa ikiwa ni njia ya kuongeza uelewa juu ya umuhimu wa ufuatiliaji wa mara kwa mara wa matibabu ili kuwawezesha wagonjwa kupatiwa matibabu stahiki na ya wakati ili kuhakiksha ugonjwa huo unatokomezwa hapa nchini.
Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika hospitali ya CCBRT, Mkurugenzi Mtendaji wa Tigo, Simon Karikari alisema “Upatikanaji wa huduma za afya kwa wagonjwa wenye ugonjwa wa mguu kifundo hasa watoto imekuwa ni changamoto kubwa hivyo tatizo hili linatakiwa kupewa kipaumbele na kwa kuona hilo Tigo tunahakikisha tunabadili historia,” alisema. Karikari alisema pia msada huo utaongeza ushiriki wa jamii na utayari wa wadau katika kuhakiksiha matibabu ya uhakika kwa watoto wenye tatizo hilo yanapatikana ili kutoa fursa kwa wao kushiriki katika shughuli za maendeleo.
Aidha, Karikari alitoa wito kwa wadau wengine kuungana na Tigo katika kuboresha maisha ya watoto wanaozaliwa na ugonjwa wa miguu kifundo kwakuwa ugonjwa huo unaweza kutibika. “Kupitia mchango huu tunaendelea kudhihirisha dhamira yetu ya kusaidia kujenga Taifa la watu wenye afya ambao wataweza kuchangia katika shughuli za kimaendeleo na pia nitoe wito kwa wadau wengine kuungana na CCBRT ili kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii yetu,” alisema. Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Brenda Msangi aliishukuru Tigo kuwa sehemu ya maendeleo ya hospitali hiyo ikiwa ni pamoja na kuboresha maisha ya wagonjwa hasa watoto.
from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2VUCbwd
via
