SOKA: Wachezaji wa Kigeni Wenye UBORA Wanaimarisha ligi Tanzania

Masama BlogKITAIFAMICHEZO5 months ago152 Views

Kuna namna wachezaji wa kigeni wenye ubora wanavyozidi kuja kwenye ligi yetu na ubora wa wachezaji wazawa unaongezeka! Inawezekana ile hoja ya kuruhusu wachezaji wachache wa kigeni ili wachezaji wa ndani wapate nafasi zaidi kwenye klabu kubwa (Simba/Yanga) haikua na mashiko

Wapo wazawa waliojipambanua kwenye klabu hizohizo kubwa wakapata namba na mwisho wa siku wanaonyesha ubora mkubwa sana kwenye timu yetu ya taifa.

Kwa tathmini fupi Mtizame Mudathir, Ibra Bacca kisha mtizame shomari na Zimbwe Jr ambae kawakimbiza ma-pro kibao kwenye namba yake….mtizame Feisal ambae alikua anapata nafasi mbele ya Azziz Ki pale Yanga….uwezo unajieleza.

SOMA HII: RC Dodoma atoa wito huu kwa Wizara ya Katiba na Sheria

Kuna namna klabu ya Azam ambayo inalisha soka la Tanzania kwa asilimia kubwa ya wachezaji kutoka kwenye mifumo yake ya soka la vijana imeleta wachezaji muhimu kama Sopu na mpishi wa mabao Nado!

Huenda kufanya vizuri kimataifa kwa klabu zetu imekua chachu ya kuwa na ligi bora? Na pia wachezaji wetu wa ndani kuimarika kwa kiasi kikubwa?

Majibu yatasalia kwenye hatua tutakayofika kwenye michuano hii ya CHAN. Ila mpaka kufikia sasa naona hata benchi la ufundi lipo na wazawa kwa 90%.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.