Shuhudia Jinsi Mama alivyomuua mwanaye kwa kumzamisha kwenye ndoo ya maji,Atiwa Mbaroni

Admin Updates1 year ago6 Views

Mwanamke aliyetambuliwa kwa jina la Johari Mbuma (19), mkazi wa Kigamboni Manispaa ya Iringa anashikiliwa na polisi akituhumiwa kumuua mtoto wake mwenye umri wa miezi saba kwa kumzamisha kwenye ndoo ya maji chooni kichwa chini miguu juu akiwa Mtaa wa Mawelewele.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu Novemba 21, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Allan Bukumbi amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo, akisema uchunguzi unaendelea.

Video ambayo Mwananchi imeiona, inamwonyesha Johari akieleza tukio hilo baada ya kukamatwa na Polisi, akisema alitoka kwao na kwenda kwa rafiki yake na baadaye alipobanwa haja aliingia chooni ambako baada ya kumaliza, alimtumbukiza mtoto kwenye ndoo nyeupe iliyokuwa na maji.

Mwenyekiti wa mtaa wa Mawelewele, Obedi Mtatifikolo amesema alipata taarifa Jumapili, Novemba 19, 2021 na alitoa taarifa polisi ambao walifika kuchukua mwili wa mtoto huyo.

 

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.