Serikali Kutoa Mikopo Kwa Wanafunzi 252,245

Admin Updates1 year ago8 Views

 Serikali Kutoa Mikopo Kwa Wanafunzi 252,245

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema ili kuwezesha na kuimarisha huduma ya utoaji na upatikanaji wa mikopo kwa Wanafunzi wa elimu ya juu wenye sifa na uhitaji, Serikali itaongeza fursa za mikopo kwa Wanafunzi wa elimu ya juu kutoka 223,201 hadi 252,245.

Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2024/2024, leo May 07,2024 Prof. Mkenda amesema “Serikali itatoa mikopo kwa Wanafunzi 84,500 wa mwaka wa kwanza ambapo shahada ya kwanza 80,000, shahada za juu 2,000, wanaosoma nje ya Nchi 500 na SAMIA Skolashipu 2,000, pia itatoa mikopo kwa Wanafunzi 157,745 wanaoendelea na masomo”

“Serikali pia itatoa ufadhili wa masomo kwa Wanafunzi 40 wenye ufaulu wa juu kwenye masomo ya sayansi hususan Wanafunzi wa kike waliohitimu Mtihani wa Taifa ya Kidato cha Sita na shahada ya awali kupitia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na itaanza kutoa ufadhili kwa ajili ya shahada za juu ikiwemo eneo la fani ya mionzi na nyuklia”


0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.