
Rais Samia akutana na Rais wa TLS Boniface Mwabukusi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma, tarehe 27 Agosti, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi, leo tarehe 27 Agosti 2025, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma.

Mazungumzo hayo yalihusu masuala mbalimbali yanayohusiana na sekta ya sheria nchini, ikiwemo nafasi ya wanasheria katika kukuza demokrasia, utawala wa sheria, na haki za wananchi.
Ikulu imesema kikao hicho ni sehemu ya jitihada za Serikali kuendelea kushirikiana na wadau wa kisheria kwa ajili ya kuimarisha misingi ya haki na uwajibikaji nchini.
Boniface Mwabukusi Ameandika Haya:
Leo nimefika Ikulu ya Chamwino kuwasilisha majumuisho ya wadau mbalimbali, ambapo tulipata nafasi adhimu ya kuzungumza na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwasilisha kwa Mukhtasari kuhusu masuala makuu ya kitaifa yanayohusu:
Mheshimiwa Rais alitusikiliza kwa makini na akatoa ahadi ya kuangalia kwa karibu mapendekezo yaliyotolewa, ili kuona namna bora ya kuyatekeleza kadri muda na mazingira yanavyoruhusu.
Aidha, kwa kuwa mapendekezo hayo yamegawanyika katika ya muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu, Mheshimiwa Rais ameahidi kuyapitia kwa ukamilifu na kuchukua hatua stahiki kwa yale yatakayowezekana, ili kuhakikisha Taifa linaingia kwenye uchaguzi ulio bora zaidi, wenye heshima, uhuru na haki kwa Watanzania wote.
BAK MWABUKUSI
SOMA ALICHOANDIKA BABA LEVO BAADA YA KUTEULIWA KUGOMBEA UBUNGE KIGOMA MJINI






