MPYAA: Elimu ya Msingi Sasa Tanzania Kuishia Darasa la Sita, Hii Kuwahusu Walioko Darasa la Tatu Mwaka huu

Admin Updates1 year ago6 Views

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema Mitaala mipya ya Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Ualimu itaanza kutumika baada ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la 2023 kupitishwa na Mamlaka za maamuzi ambapo rasimu iliyopo inapendekeza Watoto waliopo darasa la tatu mwaka huu wasome mpaka darasa la sita kisha waende Sekondari, badala ya kuishia darasa la saba.

Prof. Mkenda amesema hayo Jijini Dodoma ambapo amesema tarehe rasmi ya kuanza kutumika kwa mitaala hiyo itatangazwa baada ya kupitishwa kwa Sera hiyo na kwamba itakapopitishwa utekelezaji utaanza kwa awamu.
Mkenda amesema rasimu hiyo inapendekeza Watoto waliopo darasa la tatu Mwaka huu 2023 ndio watakaosoma mpaka darasa la sita, hivyo wale waliopo darasa la nne, tano na sita wataendelea kusoma mpaka darasa la saba.
“Hatima ya yote utekelezaji huu unategemea Mamlaka ya Nchi itakaposema tuanze, matumaini yetu ni makubwa kwamba rasimu hii itapita na siku ya kutangazwa kuanza kwa utekelezaji itakuwa ni siku kubwa katika kuelekea mageuzi ya elimu nchini”
Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.