MPYA: Hii ndiyo idadi ya Watanzania waliofariki ajali ya moto Afrika Kusini

Admin Updates1 year ago5 Views

Idadi ya Watanzania waliofariki katika ajali ya moto iliyotokea Alhamisi wiki iliyopita nchini Afrika Kusini, imeongezeka hadi kufikia 6 huku zoezi la kutambua miili likiendelea.

Akizungumza katika mahojiano na kituo cha televisheni cha Azam, Balozi wa Tanzania nchini humo, Meja Jenerali mstaafu, Gaudence Milanzi, amesema idadi ya vifo imeongezeka kutoka 74 hadi 77.

“Suala la utambuzi linaendelea na limetokana na ushirikiano kati ya ubalozi na maafisa wa Serikali ya Afrika Kusini, mpaka sasa tumetambua miili sita za Watanzania,” amesema Milanzi.

Kuhusu taratibu za kusafirisha miili ya Watanzania hao kwa ajili ya maziko nchini, Balozi Milanzi amesema kuwa bado hawajaanza taratibu hizo, isipokuwa wameanza kufanya taratibu za kujua ndugu wa waliofariki.

“Hatuwezi kusafirisha kabla hatujajua ndugu zao ni kina na nani, tukikamilisha hilo ndipo tutatangaza utaratibu mzima wa kusafirisha,” amesema balozi huyo.

Aidha amesema majeruhi Watanzania wanaendelea vizuri kufuatia huduma ambazo wamekuwa wakipatiwa na Serikali nchini humo.

Pia amesema Serikali hiyo imewapatia hifadhi waliokuwa wakiishi katika jengo ambalo liliungua moto huku baadhi ya waathiriwa wakikataa kuhifadhiwa kwa kuhofia kukaguliwa uraia wao.

“Wengine hawakupenda kuhifadhiwa, hatujui hata wako wapi. Wana hofu ya kumatwa kwa kutokuwa na vibali. Waliokubali wanaendelea kupata huduma za afya na vyakula,” ameongeza.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.