Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Meninah
Abdulkareem ‘Meninah’ amefunguka juu ya tetesi zinazoeneo kuwa na
uhusiano wa chinichini na Nasib Abdul ‘Diamond’ kwa kusema kuwa siyo
levo yake.
Akichonga na paparazi wetu, Meninah anayetamba na ngoma ya Pipi ya
Kijiti alikanusha na kusema kuwa, wote ni mastaa lakini wametofautiana
kwa kiasi kikubwa na kwamba hawezi kuwa naye katika mahusiano ya aina
yoyote.
“Kwanza nilishawahi kukutana naye kwenye shoo tofauti na zote
sikuwahi hata kuzungumza naye chochote, ni staa na mimi staa lakini
tunatofautiana kuwa yeye yupo juu yangu,” alisema Meninah.