MAKAMU WA RAIS ASEMA UPATIKANAJI WA MAJI KALIUA KUFIKIA ASILIMIA 50 MWAKA 2020

7 years ago97 Views

NA TIGANYA VINCENT

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itahakikisha tatizo la maji wilayani Kaliua linatafutiwa ufumbuzi ili kuwatua ndoa kichwani wakinamama.

Alisema ifikapo mwaka 2020 hali ya upatikanaji wa maji katika Wilaya ya Kaliua utaongezeka kutoka asilimia 25 za sasa na kufikia asilimia 50

Makamu wa Rais alitoa kauli hiyo kwenye mkutano wa hadhara katika uwanja wa Kolimba wilayani Kaliua ikiwa ni siku nne ya ziara yake mkoani Tabora .

Alisema Serikali itahakikisha inachimba visima na kujenga mabwawa katika maeneo ambayo maji kutoka Ziwa Victoria yatakaposhindwa kufika ili kuwaondelea shida na upatikanaji wa maji safi na salama wananchi.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais ametoa onyo kwa watu ambao wameanza kuingia katika hifadhi za mistu na kuendesha uharibifu ikiwa ni pamoja na ukataji wa miti na kuendesha kilimo ndani ya hifadhi.

Alisema tamko la Rais wa Jamhuri ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli lilihusu vijiji ambavyo vilikuwa tayari ndani ya maeneo ya hifadhi na vilivyo ainishwa na sio kuanzisha makazi mapya ndani ya hifadhi.

Makamu wa Rais alisema mtu akayeingia katika Hifadhi atachukuliwa hatua za kisheria na kuwataka Watendaji mbalimbali kuhakikisha wanawaondoa watu ambao wameanza kuvamilia mistu na kuongeza kuwa Rais Magufuli hakusema watu waanze kuingia katika hifadhi ya mistu.

Wakati huo huo Makamu wa Rais alisema ifikapo mwaka 2023 vijiji vyote nchini vitakuwa na umeme. Aliwataka wananchi kutumia upatikanaji wa umeme katika masuala ya maendeleo ya viwanda vya kati na vikubwa.

from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2H5dR58
via

Previous Post

Next Post

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.