Haya hii ya leo ngoja niwatobolee siri kidogo tu kwenye upande wa
mapenzi. unajua wanawake bwana tupo kama mayai ukiyaminya kidogo tu huwa
yanapasuka.. sasa wengi wanaume huwa wanabaki kuropoa “wanawake
hawaeleweki” WANATAKA TUWEJE? Mwanamke huwa anapenda sana kuambiwa
ukweli japo wengi wanadai eti bila kudanganywa hatuingiliki, Wanawake
wengi hupenda kuspend muda wake zaidi na wake mpenzi
uliko na marafiki zake. Mwanamke hupenda mwanaume anaejali zaidi kuliko
mbabaishaji “sasa wewe jifanye gogo tuone kama utapata mrembo” Jeuri
ufanyiapo mwanamke dhahir huwa unamvunja moyo na hukushusha thamani yako
pindi umfanyiayo yakawa yale yanayo mdharaulisha zaidi Mthamini mpenzi
wako hata ukiwa na watu wengi, onyesha unajali kuwa nae karibu, hujiona
wa pekee Mwanamke hupenda kusikilizwa japokuwa wanaume hujifanya vichwa
na kutuona hatuna la kuongea lakini sio kweli ni fikra zenu tu.
Msikilize mpenzi wako uone kama na wewe
hatokusikiliza Mwanamke huthamini sana msg za mpenzi wake kuliko simu
apigiwayo na mwenza wake, maana kuona faraja zaidi pindi asomapo msg
hizo zaidi ya kupoteza muda kusubiri apigiwe au akupigie. Msifie mkeo
ama mchumba wako pindi apendezapo na kumpa faraja pindi aumizwapo.
Msikilize mchumba wako na usitumie lugha ya ukali akuombapo ushauri bali
jaribu kuchunguza zaidi nini atakacho kwako. Kila lililo dogo usilikuze
bali lipe nafasi yake katika kutoa kipingamizi ama makubaliano.lasivyo
utasababisha kutokujiamini.
Onyesha unajali Mkumbuke kila wakati hata mara 2 kwa siku Punguza jeuri
na kauli chafu ukifananya kati ya hayo hutopata misukosuko mingi na
kumbuka kujishusha endapo ufanyapo kosa na acha kutumia mabavu zaidi
kuliko upole. haya jamani ni hayo tu labda utaona umuhimu wa mwenza wako
zaidi ya kuliko kutoa lawama juu yake, wapendwa kama hamtojali kama
kuna ambayo wakina kaka nao wanataka kutoa kero zao uwanja wenu