Mahakama Kuu ya Kenya Yamzuia Ruto Kujenga Kanisa

Masama BlogKIMATAIFASIASA3 months ago208 Views

Mahakama Kuu ya Kenya Yamzuia Ruto Kujenga Kanisa

KAMA Kuu nchini Kenya imetoa agizo la muda ya kuzuia ujenzi wa Kanisa au majengo yoyote yenye mafungamano ya dini ndani ya viunga vya Ikulu ya Nairobi, hatua inayokuja baada ya makundi manne ya kiraia kufungua pingamizi wakidai kuwa ujenzi wa jengo la kidini katika eneo la taasisi ya taifa ni kinyume cha sheria na kanuni za utawala bora.

Uamuzi huo umetolewa na Jaji wa Mahakama Kuu, Chacha Mwita ambaye amesema ujenzi huo usitishwe kwa muda hadi pale hukumu ya mwisho itakapotolewa mwezi Novemba 2025 hatua ambayo ni kama ushindi wa muda kwa wanaharakati wa kiraia, huku ukiweka shinikizo jipya kwa serikali kueleza iwapo hatua hiyo inaheshimu misingi ya kikatiba na usawa wa kidini nchini Kenya.

Hivi karibuni Rais wa Nchi hiyo William Ruto alinukuliwa hadharani akisema ameagiza kujengwa kwa Kanisa hilo kwa kutumia fedha zake binafsi, jambo lililozua mijadala mikubwa miongoni mwa wananchi na wadau wa kisheria huku wakosoaji wakisema hata kama fedha ni za binafsi, ujenzi ndani ya lkulu unaweza kufupisha mipaka kati ya dola na dini na hivyo kuibua mgongano wa kikatiba.

SOMA HIZI:

Unahitaji Ushinde Zabuni?Je Unakwama wapi?Soma HAPA

Mgombea wa CCM Ruangwa aandika haya Kuelekea uzinduzi wa Kampeni za CCM Kitaifa

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...