KOCHA Jurgen Klopp aagwa kwa heshima Liverpool

Admin Updates1 year ago4 Views

 KOCHA Klopp aagwa kwa heshima Liverpool

Mabao ya kipindi cha kwanza ya Alexis Mac Allister na Jarell Quansah yamemfanya Jurgen Klopp kumaliza kibarua chake cha kuinoa Liverpool kwa heshima.

Mashabiki wa Liverpool wamefurika kwenye Uwanja wa Anfield kumshukuru Klopp ambaye leo Jumapili, Mei 19, 2024 alikuwa akiwaongoza wababe hao wa Ulaya kwenye mchezo wa mwisho.

Tayari Klopp alishatangaza kuachana na Liverpool mwishoni mwa msimu ambao umefikia tamati leo, akitaka kutumia muda zaidi na familia yake.

Liverpool imemaliza Ligi Kuu ya Uingereza ikiwa nafasi ya tatu nyuma ya Arsenal, kwa kuichapa Wolverhampton mabao 2-0. Katika mchezo huo Nelson Semedo alimaliza msimu kwa kulimwa kadi nyekundu na kuifanya Wolves kucheza pungufu.

Akiwa na Liverpool, Klopp amebeba mataji ya EPL, Ligi ya Mabingwa Ulaya, Klabu Bingwa Dunia na Super Cup.


Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.