Huu hapa uamuzi wa simba kuhusu Juma mgunda

Admin Updates10 months ago6 Views

 

Kaimu Kocha Mkuu wa Simba Juma Mgunda amehakikishiwa na mabosi wa timu hiyo ataendelea kubaki katika benchi la ufundi hata ikitokea mabadiliko katika nafasi yake


Mgunda anawindwa na klabu ya Coastal Union ambayo inamuhitaji kwa ajili ya kujiimarisha kuelekea michuano ya kombe la Shirikisho msimu ujao

Wakati Simba ikiwa bado haijatangaza hatma ya benchi la ufundi, usajili unaofanyika sasa umetokana na ripoti ya makocha Abdelhak Benchikha na Mgunda ambaye ndiye aliyemaliza msimu akiwa Kocha Mkuu

Litakuwa jambo la kushangaza kama Simba itaachana na Mgunda na kuleta watu wapya katika benchi la ufundi ambao hawafahamu masuala mengi kuhusu klabu

Na pengine hii ndio sababu uongozi umeona lazima Mgunda abaki hata kama kwa nafasi ya Kocha Msaidizi ikitokea mabadiliko katika nafasi ya kocha mkuu

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amesema taarifa kuhusu benchi la ufundi itatolewa wakati wowote kabla ya kikosi kuelekea Misri wiki ijayo
Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.