HATAREEE:WASANII DIAMOND, ALI KIBA UCHAWI WATAWALA, HIRIZI ZAOKOTWA UWANJANI MOJA YAKUTWA IKIPUMUA

Admin Updates10 years ago5 Views


HALI inazidi kuwa mbaya kwa mastaa wawili wa muziki wa Bongo Fleva
wanaogombea unyota kimuziki, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Ali
Saleh Kiba, safari hii yameibuka mapya kwa kila msanii kuogopa kumshika
mkono mwenzake kutokana na imani za kishirikina.

TUJIUNGE LEADERS
Matukio hayo ya kusisimua yaliwatia hofu kubwa mashabiki na wadau wa
muziki Bongo muda mfupi kabla ya nyota hao kukaribishwa stejini kwenye
Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar, mwishoni mwa wiki
iliyopita.

HIRIZI ZAKUTWA UWANJANI
Kwa mujibu wa wanahabari wetu, katika Viwanja vya Leaders, Kinondoni,
kulikutwa hirizi zilizozagaa, zilizodaiwa kudondoshwa  na vijana
waliokamatwa wakiwa wamevalia sare zenye majina ya mastaa hao wawili.

Katika hali ya kushangaza, mmoja wa mashabiki waliohudhuria onyesho hilo
ambaye aliziona hirizi hizo, aliwashangaza mashabiki wenzake alipodai
kuwa anaiona mojawapo ikitweta mithili ya inayopumua!
“Oneni wadau, hii hirizi si inapumua, iangalieni vizuri,” alisikika
shabiki huyo na kuwaacha watu wakiwa wamepigwa na butwaa kuona vitendo
hivyo vya kishirikina katika eneo la burudani.



Wakati matukio hayo ya kukutwa kwa hirizi hizo yakiendelea, Diamond,
baada ya kupanda jukwaani kabla ya kuanza kuimba, akajikuta akiteleza na
kuanguka jukwaani na kusimama mwenyewe huku vijana wanaodaiwa kuwa ni
wa Timu Kiba wakipiga kelele kwa nguvu kuashiria kuwa walipendezewa na
kitendo hicho kutokea.

Pamoja na Diamond kula mwereka hadi chini, hali ilizidi kuwa mbaya kwake
baada ya muziki kuanza kusikika vibaya huku ukiwa unakatakata, kitendo
kilichoamsha hisia kuwa kulikuwa na ushirikina unaoendelea ili kumshusha
kisanii kwa kuonekana amefanya vibaya katika shoo hiyo

CHUPA ZARUSHWA
Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya huku chupa za maji zikirushwa
jukwaani hapo na baadhi zikimpiga na nyingine akizikwepa wakati
akiendelea kupiga shoo, Diamond aliamua kutumia akili ili kuzima kelele
hizo kwa kuanza kumwaga noti.

Ishu hiyo iliwafanya mashabiki na Timu Kiba kuachana na zoezi hilo na
kuanza kusukumana kugombea noti hizo za elfu mbilimbili ambapo alimwaga
kwa awamu tatu.

SADAKA?
Wakati akizidi kuwatupia noti mashabiki, Diamond alisikika akisema kuwa
pesa hizo ni maalum kwa mashabiki kwani ni sadaka kwao kutokana na
sapoti kubwa wanayompa ingawa hataweza kumpa kila mmoja.

DIAMOND KAMA MICHAEL JACKSON
Hata hivyo, baadhi ya mashabiki waliokuwa wakisukumana na kuokota noti hizo walisikika wakisema:
“Huu mchezo alikuwa akiufanya Michael Jackson (Mwanamuziki marehemu wa Marekani) tena alikuwa akitumia ushirikina na Freemasons.
“Michael alikuwa anadaiwa kumwaga fedha hizo zilizokuwa na nguvu ili
kuwafanya wale waliokuwa wakimzomea kukaa kimya,” alisikika shabiki
mmoja akisema.

MSHANGAO
Katika hali ya kushangaza zaidi,  Diamond alivua tisheti na vesti ya
ndani na kujifuta jasho kisha kuwarushia mashabiki huku akijua wazi kuwa
amefutia jasho lililokuwa likimiminika mwilini mwake kama maji.

KIBA HAKUTAKIWA KUZUNGUMZA?
Wakati matukio ya kushangaza aliyokuwa akiyafanya Diamond na yale ya
kurushiwa chupa za maji machafu na yenye mikojo yakiendelea, ilidaiwa
kuwa Kiba alipoingia kwenye chumba cha wasanii hakutaka kuzungumza na
mtu yeyote huku ikidaiwa kuwa hiyo ni ishara kubwa kuwa hakutakiwa
kuzungumza na mtu kwani angeweza kupoteza nguvu za kufanya shoo.

POLISI MZIGONI
Wakati mashabiki wakizidi kuwa na wasiwasi juu ya wasanii hao, jeshi la
polisi lililokuwa na zana zote za kukamatia wahalifu, walianza doria ya
kukamata vijana ambao wanadaiwa kuwa ni Timu Kiba waliokuwa wakibishana
na kutupa chupa zenye mikojo na maji  huku wakipokea kipigo kama cha
mbwa mwizi.

KIBA ARUKA UKUTA
Awali kabla ya shoo hizo kuanza matukio ya kishirikina yalijidhihirisha
zaidi baada ya Ali Kiba kuingia uwanjani hapo kwa njia ya kuruka ukuta
na hata alipozama kwenye chumba maalum walichokuwa wametengewa wasanii
hakuweza kushikana mikono na wenzake.Wasanii ambao Ali Kiba aliwachunia
ni AY, MwanaFA, Shaa, Shilole, Vanessa Mdee na Jux, ambao wote aliwakuta
ndani ya chumba hicho.

Imeandaliwa na Gladness Mallya, Musa Mateja, Chande Abdallah, Mayasa Mariwata, Shani Ramadhani, Denis Mtima na Laurent Samatta

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.