Mbunge wa Ukonga na Waziri wa ardhi Mhe. Jerry Silaa akimsikiliza Mama Lishe huyu ambaye ni Mmoja wa wapiga Kura wake ambaye pia mama lishe huyo amempongeza kwa kuaminiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Taznania Mhe.Samia Suluhu Hassan na kumteua kuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwani wao kama wananchi wa Ukonga wanaamini ni bahati kwao na ina tija kubwa kuwa na waziri ambaye anaamini atakuwa mmoja wa watatuzi muhimu wa Migogoro ya Ardhi Nchini ikiwepo jimbo la Ukonga.
Waziri Jerry Silaa akiondoka kwa Mama lishe huyo baada ya kumsikilza na kupata mihogo kama Chakula chake cha mchana huku akiisifia kwa kusema watu wengi hawajui kama mihogo ni moja ya chakula bora na kinacholiwa sana na watu wengi hasa maeneo ya mijini na vijijini kwani yeye tangu akiwa shule ya msingi,sekondanri hata vyuo kwake Mihogo ni moja ya chakula anachokipenda sana