Muuza sura kwenye sinema za Kibongo, Fatuma Ayubu ‘Bozi’.
MUUZA sura
kwenye sinema za Kibongo, Fatuma Ayubu ‘Bozi’ ambaye alikiri kubanjuka
na mastaa wasiopungua 15, amesema sababu zinazomsababisha asidumu na
mwanaume mmoja kwenye mapenzi ni kutokana na mateso aliyoyapata kwenye
ndoa ya utotoni.
Akibonga mawili matatu na paparazi wetu, Bozi alisema tatizo la
kutokuwa na msimamo kwenye mapenzi linatokana na kuumizwa na mwanaume
ambaye alimuamini na kuingia naye kwenye ndoa, ambapo aliambulia vipigo
na mafumanizi ya mara kwa mara.
“Ukweli mshipa wa kupenda umeshanikatika, nikiwa na mwanaume kwa kipindi
kifupi tu namchukia na kusitisha uhusiano, chanzo kinatokana na
mwanaume ambaye alinibembeleza anioe nikiwa na umri wa miaka 17 tu na
kila siku kufuma SMS za wanawake na hata kumshuhudia, nilichoambulia ni
mtoto ambaye jukumu zima la malezi ni mimi mwenyewe,” alisema Bozi.