Benson Kigaila: Si Lazima Mbowe Kwenda Mahakamani Kesi ya Tundu Lissu

Masama BlogSIASA6 months ago186 Views

Benson Kigaila: Si Lazima Mbowe Kwenda Mahakamani

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Bara, Benson Kigaila ameeleza kuwa si lazima kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe kushiriki vikao vya CHADEMA kwasababu yeye ni mwanachama wa kawaida.

Akizungumza na Wilberforce Ngoto @wilberforcengoto8218 wa kipindi cha Maswali na Majibu kinachorushwa na Jambo TV, Kigaila amesema kuwa mwanachama wa kawaida wa CHADEMA hushiriki mkutano mkuu wa tawi kwenye tawi lake.

Aidha ameeleza kuwa Mbowe amekuwa akifanya mambo kwa ajili ya CHADEMA bila kujionesha ikiwamo kuwasiliana na kumuona Mwenyekiti wa chama hicho taifa Tundu Lissu gerezani, likiwa ni jibu kwa baadhi ya Watanzania ambao wamekuwa wakihoji kutoonekana kwa Mbowe katika viunga vya mahakama kufuatilia kesi zinazomhusu Lissu na CHADEMA.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.