Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, akizungumza katika hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya Barclays Tanzania kwa wateja wake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Barclays, Aron Luhanga (kushoto), akizungumza na Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum (kulia), pamoja na Mkurugenzi wa Habari katika Ofisi ya Shehe wa Mkoa, Tabu Kawambwa katika hafla hiyo.
Meneja Huduma za Jamii wa Benki ya Barclays Tanzania, Hellen Siria (kulia), akisaidia kugawa mlo wa futari kwa baadhi ya waalikwa katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Barclays Tanzania, Abdi Mohamed (katikati), pamoja na baadhi ya wageni waalikwa wakifuturu katika hafla iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wao jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Baadhi ya wageni waalikwa wakishiriki mlo wa futari uliondaliwa na Benki ya Barclays Tanzania jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
from MICHUZI BLOG http://bit.ly/2JQOANC
via





