Ally Kamwe : Yanga Tunakwenda Kuonesha Dunia Jinsi Gani Tunamfunga Al Ahly

Admin Updates1 year ago5 Views

Baada ya kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Simba SC, uongozi wa Young Africans umesema kuwa sasa ni zamu ya Mabingwa wa Soka Barani Afrika Al Ahly ya Misri kuhakikisha kuwa wanapokea kichapo kutoka kwao katika michezo ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika pindi watakapokutana.
Young Africans watakutana na Al Ahly katika michezo ya Ligi ya Mabingwa Afrika Kundi D ambalo linawajumuisha vigogo hao wawili pamoja na CR Belouzdad kutoka Algeria na Madeama kutoka Ghana.
Ofisa Ally Kamwe alisema: “Baada ya kuwafunga Simba SC sasa tunataka kwenda kuionyesha dunia ni namna gani Young Africans tutamfunga Al Ahly ambao walishindwa kufungana na Simba SC katika michezo waliyokutana nao.
Young Africans msimu huu tumedhamiria na tunataka kuhakikisha kuwa tunafika mbali katika michuano hii ya kimataifa ambayo watu wanatuona kama hatuwezi kufanya kitu.
“Tuna malengo makubwa ambayo tutawaonyesha watu baada ya kufanikiwa, kwa sasa hatutaki kuongea sana kwa kuwa watu hawawezi kutuelewa lakini Young Africans hii niwahakikishie mashabiki wetu kuwa watafurahi sana,” amesema Kamwe.

 

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.