MREMBO aliyewahi kuwa na uhusiano na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Faiza Ally, mwanzoni mwa wiki hii aliamriwa na Mahakama ya Manzese/Sinza, amkabidhi mtoto kwa baba yake (Sugu) ambaye aliiomba mahakama hiyo imruhusu apewe mtoto huyo kwa madai kuwa mama yake huyo anamlea kinyume na maadili.
Sugu aliileza mahakama kuwa mrembo huyo hana maadili kwani amekuwa akijipiga na kumpiga picha za nusu utupu mtoto na kuziweka mitandaoni kitu ambacho aliamini kitamsababishia akose maadili.
Mara baada ya hukumu hiyo kutolewa, Mikito Nusunusu ilimtafuta Faiza na kutaka kujua ameipokeaje pamoja na historia nzima ya yeye kukutana na mzazi mwenzake huyo, shuka na mtiririko wa maswali na majibu:
Alianza lini kuvaa mavazi ya nusu utupu?
“Jamani haya mavazi wanayosema navaa uchi sijaanza kuvaa leo ni tangu utotoni, hakuna ambaye hajui kitu hicho kwa kuwa hata mama yangu alikuwa akinishonea sketi ya shule ndefu mimi naenda kwa fundi kuikata.”
Alikutana vipi na Sugu?
“Nilikutana naye kwenye Mtandao wa Facebook na alikuwa akiniona nikiwa katika mavazi hayohayo ambayo yeye anadai ni ya kuvunja maadili na alinitongoza nakumbuka nilikuwa Zanzibar kwenye hoteli moja inaitwa Lagema, ambapo nilitupia picha zangu zilezile ndipo alipovutiwa nazo akarusha nyavu.”
Hakumpa masharti ya nguo anazopenda?
“Yeye aliniambia kuwa kama ‘package’ amepata iliyokamilika kuanzia mavazi yangu ninayovaa mpaka ‘tatoo’ nilizochora hivyo alinikubali kwa jinsi nilivyo.”
Anazungumziaje kuvaa nguo fupi?
“Jamani ninachoamini mimi nguo siyo kila kitu katika maisha ya mtu, mimi ni mama wa tofauti kwa mtoto wangu hilo hata Sugu mwenyewe analijua kabisa, nimeanza kumfundisha mtoto wangu kusoma kabla hata hajaanza shule na si mtu wa kujirusha kama wanavyofikiria.”
Kumbe vimini vilianzia kwenye filamu
“Kabla sijawa na Sugu, nilikuwa na filamu yangu inaitwa Jesca, nafikiri ndiyo muigizaji wa kwanza kuvaa bikini na kutembea hadharani lakini yote hiyo ni kutokana na mazoea, hata Sugu aliiona filamu hiyo, hakuona kama ni ukosefu wa maadili.”
Alitinga ‘swimming’ akiwa na mama mkwe
“Nakumbuka mimi na mama yake Sugu tulishawahi kwenda ufukweni nikiwa na mtoto wangu na nilikuwa nimevaa nguo za kuogelea na wala haikuwa tatizo na siyo mama hata nikiwa naye mara nyingi navaa hivyo, nashangaa sasa anasema navunja maadili.”
Sugu alimkuta akiwa na maisha mazuri?
Recommended Products
-
2025 Summer Rapper Feid Ferxxo Men’s Cotton Fashion Hip-hop T-shirt Casual and Comfortable Short-sleeved T-shirt Street Wear
Affliate products $22.00 -
3 IN 1 Magnetic Folding Wireless Charger Station For IPhone Transparent Fast Charging For IWatch And Airpods
Affliate products -
Grandpa Of Love hoodies Human French Letters Dad Papa Papy Gift Men Clothing hoodies
Affliate products $22.00 -
Sale!
Lenovo D18 Drone 8K Aerial HD Dual-Camera Intelligent Obstacle Avoidance Brushless Power 5G WIFI Screen Remote Control GPS Drone
Affliate products Original price was: $7.99.$7.89Current price is: $7.89. -
Mini Portable Face Cordless Shavers Rechargeable USB Electric Shaver Wet & Dry Painless Small Size Machine Shaving For Men
Affliate products $44.00 -
New Original T75 Bone Conduction Wireless Bluetooth 5.3 Headphones Sports Earphones HiFi Sound Quality Waterproof TWS Headset
Affliate products $3.33












