LOL! Kumbe suala la kuolewa Ray C alikuwa anajaribisha tu kuona kama mashabiki wake mpo.
“Hapana sina mpango wa kuolewa, mme mwema anatoka kwa Mungu, huwezi
sema unatangaza. Sasa hivi sipo kwenye mahusiano sina mtu, nikimpata
mtasikia. Kuhusu kutafuta mme wa kunioa huo ulikuwa utani tu, nilikuwa
nataka kuwafurahisha watu wangu wa insta. Nimepokea simu nyingi zaidi ya
500 hadi saa 6 usiku. Kwahiyo nimeona mashabiki bado wapo na
wananipenda. amesema Ray C