MASTAA SHILOLE NA NUH MZIWANDA MIKONONI MWA POLISI
9 years ago91 Views
Share
Shilawadu wamezinyaka za chini ya carpet kuwahusu wasanii wawili wa Bongo Fleva Shilole na Nuh Mziwanda kuwa wameshikiliwa na Jeshi la Polisi huko Kahama mkoani Shinyanga.
Kwa kile kinachosemekana kuwa Nuh Mziwanda alitaka kumtapeli promota ambaye walikuwa wamekwisha kubaliana na kulipana pesa kwa ajili ya kufanya show na baadaye Nuh Mziwanda kutaka kutopiga show hiyo na badala yake kwenda kupiga show nyingine ambayo iliandaliwa na Shilole.
Soudy Brown amepiga story na Promota huyo pamoja na Nuh Mziwanda na wamefugnuka jinsi mchongo mzima ulivyokuwa.