Simba Wamaliza Kazi iliyowapeleka Zanzibar, Al Ahly Hawatoboi Zindiko Limekubali

Admin Updates1 year ago5 Views

 Simba Wamaliza Kazi iliyowapeleka Zanzibar, Al Ahly Hawatoboi Zindiko Limekubali

Kikosi cha Simba SC kimeanza safari ya kurejea jijini Dar es salaam kikitokea kisiwani Unguja, Zanzibar baada ya kumaliza kambi ya maandalizi ya Mchezo wa Mkondo wa Kwanza wa Robo Fainali, Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.
Simba SC itakuwa mwenyeji wa mchezo huo utakaowakutanisha dhidi ya Mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Al Ahly kutoka nchini Misri, utakaopigwa Ijumaa (Machi 29) Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es salaam.
Kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya Simba SC wachezaji wa Simba SC wameonekana wakiwa bandarini kisiwani Unguja, tayari kwa safari ya kurejea Dar es salaam.
Hata hivyo Simba SC inatarajiwa kuendelea na maandalizi ya mchezo huo ikiwa jijini Dar es salaam, huku wapinzani wao wakitarajiwa kuwasili nchini kesho Jumatano (Machi 27).
Ikumbukwe kuwa Mshindi wa jumla wa mchezo huo atatinga Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika na atakutana na Mshindi wa mchezo katia ya Petro Atletico (Angola) dhidi ya TP Mazembe (DR Congo).

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K

Stay Informed With the Latest & Most Important News

I consent to receive newsletter via email. For further information, please review our Privacy Policy

Categories
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.