Rais Samia Aitaka Simba ijipange Msimu ujao Baada ya Kutolewa Robo Fainali CAF

2 years ago115 Views

 Rais Samia Aitaka Simba ijipange Msimu ujao Baada ya Kutolewa Robo Fainali CAF

Rais Samia Suluhu Hassan ameitaka Simba ijipange kwaajili ya msimu ujao wa Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kutolewa kwenye robo fainali ya michuano hiyo na bingwa mtetezi Al Ahly leo kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Cairo, Misri

Rais Samia ameandika kwenye mitandao yake ya kijamii “chezo mzuri Simba. Usiku haukuwa wa ushindi lakini tumeziona juhudi na zinatupa faraja na matarajio kuwa, msimu ujao wa mashindano ya Ligi ya Mabingwa ya Shirikisho la Soka Afrika mambo yatakuwa mazuri zaidi. Ahadi yetu ni kuendelea kuwaunga mkono na kuwapa motisha.”

Simba imeishia Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika mara ya nne katika misimu sita baada ya kupokea kichapo cha jumla ya mabao 3-0 na Al Ahly bingwa mtetezi wa michuano hiyo.

Simba imepoteza ugenini mabao 2-0 Cairo yakifungwa Amr El Solia dakika ya 47 na Mahmoud Kahraba kwa penalti dakika ya 90 huku bao la kwanza lilifungwa na Ahmed Nabil Koka Machi 29, katika Uwanja wa Mkapa.

Previous Post

Next Post

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.