ZAHERA AONDOKA..AOMBA ASIULIZWE CHOCHOTE

7 years ago92 Views

Kocha Mwinyi Zahera akiwa na wachezaji wa Yanga.

Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera baada ya mchezo wa jana dhidi ya KMC ambapo Yanga ilishinda mabao 2-1, ameaga kuwa anaondoka nchini kuelekea kwao DR Congo.

Zahera anakwenda DR Congo kwaajili ya majukumu ya timu ya taifa ambayo yeye ni kocha msaidizi huku akisisitiza kuwa taifa lake lina mchezo mgumu sana dhidi ya Liberia kuwania kufuzu AFCON 2019.

”Naenda Congo, tupo na mechi ngumu sana, nisiulizwe chochote kuhusu Simba au Yanga nawaachia namba ya kocha msaidizi Noel Mwadila mtamuuliza yote mimi sitamjibu hata mtu mmoja”, amesema.

Zahera anaondoka nchini kesho Jumanne Machi 3, 2019, lakini hajaweka wazi kama anaondoka na mshambuliaji Heritier Makambo ambaye alitajwa katika kikosi cha wachezaji 40 wa awali kuelekea mchezo huo.

DR Congo ipo kundi G ambalo linaongozwa na Zimbabwe yenye pointi 8, Liberia yenye pointi 7 huku DR Congo wakiwa na pointi 6 wakati Congo Brazzaville wakiwa na pointi 5.

from MALUNDE 1 BLOG https://ift.tt/2u1DFaO
via

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.