

Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira Vijana na wenye ulemavu Mhe.Ridhiwani Kikwete amehudhuria na kuhutubia kongamano la 9 la ununuzi wa Umma Nchini lilioandaliwa na Mamlaka ya Ununuzi wa Umma Nchini (PPRA). Akizungumza katika kongamano hilo lilianza tarehe 13/6/2025 kwenye kituo cha kimataifa cha mikutano AICC jijini Arusha amesema anaipongeza sana PPRA kwa kuandaa kongamano hilo ambalo kwa mwaka huu limebeba dhima ya “Ununuzi wa wa Umma Kidijitali kwa Maendeleo Endelevu:Ukuzaji wa Kampuni za wazawa na makundi Maalum kwa Ukuaji Uchumi Jumuishi”

Aidha Mhe Ridhiwani amemshukuru Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Mamlaka ya Ununuzi wa Umma (PPRA) kuendelea kutekeleza kazi zake kwa kuwezesha elimu ya fursa zilizopo kwa makundi Maalum,Vijana na wenye ulemavu ambao kwa sasa ni moja ya wadau wakubwa wa unufaika wa 30% ya PPRA kwenye mfumo wa NeST unaolenga kuwapa nafasi ya kufanya kazi mbalimbali za ununuzi wa Umma.
Ndugu Washiriki na Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi,Naomba niwashukuru sana kwa kutenga Muda wenu na kuhudhuria kongamano hili Muhimu la kitaaluma ambalo litaendelea kufungua fursa zilizopo katika eneo la manunuzi kwa Makundi Maalum,Vijana na Wenye Ulemavu..” kitu ambacho kitaleta tija kwa makundi hayo,wananchi na Taifa kwa ujumla..” alimalizia Waziri Kikwete






