WAZIRI AAGIZA WANASIASA WAHUNI WANAOMTUKANA RAIS MAGUFULI WAKAMATWE

7 years ago93 Views

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola ameagiza kuchukuliwa hatua za kisheria kwa wanasiasa ambao wanafanya mikutano ya ndani ambayo imepigwa marufuku.

Kangi Lugola ametoa kauli hiyo akiwa Mkoani Morogoro wakati akizungumza na wananchi wa Mjini Kilosa ambapo amesema ana taarifa za kuwepo kwa baadhi ya wanasiasa wa upinzani wanaofanya vikao vyao vya ndani huku wakitoa kauli ambazo zinaashiria uchochezi.

“Mimi Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, sitakubaliana na kiongozi wa chama chochote kuvunja agizo tulilolitoa nchi nzima kwa kutoruhusu kufanyika mikutano ya hadhara ya siasa, na pia kupitia mikutano ya ndani ambayo inafanyika, baadhi ya wanasiasa wahuni wanamtukana Rais ambaye ndiyo kiongozi Mkuu wa nchi, mimi sitakubaliana na hilo,” amesema Lugola.

Aidha Lugola amesema Rais Magufuli ni kiongozi ambaye kwa muda mfupi ameiletea mabadiliko makubwa nchi na pia ana mipango mikubwa ya maendeleo yanayokuja katika uongozi wake.
Chanzo – EATV

from MALUNDE 1 BLOG https://ift.tt/2VSkdJv
via

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.