Watuhumiwa wa Utekaji na Mauaji ya Mwanafunzi wa Mzumbe Wauawa
Watuhumiwa watatu wa utekaji na mauaji ya mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Ndaki ya Mbeya, Shyrose Mahande, wamefariki dunia baada ya kujeruhiwa kwa risasi walipojaribu kutoroka wakiwa chini ya ulinzi wa polisi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Benjamin Kuzaga, amesema tukio hilo lilitokea wakati jeshi hilo likiendelea na ufuatiliaji kufuatia mauaji ya Shyrose yaliyotokea Septemba 14, 2025.
Amesema mnamo Septemba 24 na 25, polisi walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao watatu waliotajwa kwa majina ya Marwa Nyahega, Edward Kayuni na Websta Mwantebele, lakini walipata majeraha ya risasi baada ya kujaribu kutoroka na baadaye kufariki dunia.
Kamanda Kuzaga ameongeza kuwa, licha ya vifo vya watuhumiwa hao, jeshi la polisi linaendelea na msako wa kuwatafuta wahusika wengine, akiwemo mganga wa kienyeji anayedaiwa kuhusishwa kwa kupelekewa baadhi ya viungo vya marehemu Shyrose, aliyenyongwa na kisha kuchomwa moto.
Ahmed Ally Afunguka Baada ya Kufungwa na Yanga
Recommended Products
-
2025 Summer Rapper Feid Ferxxo Men’s Cotton Fashion Hip-hop T-shirt Casual and Comfortable Short-sleeved T-shirt Street Wear
Affliate products $22.00 -
3 IN 1 Magnetic Folding Wireless Charger Station For IPhone Transparent Fast Charging For IWatch And Airpods
Affliate products -
Grandpa Of Love hoodies Human French Letters Dad Papa Papy Gift Men Clothing hoodies
Affliate products $22.00 -
Sale!
Lenovo D18 Drone 8K Aerial HD Dual-Camera Intelligent Obstacle Avoidance Brushless Power 5G WIFI Screen Remote Control GPS Drone
Affliate products Original price was: $7.99.$7.89Current price is: $7.89. -
Mini Portable Face Cordless Shavers Rechargeable USB Electric Shaver Wet & Dry Painless Small Size Machine Shaving For Men
Affliate products $44.00 -
New Original T75 Bone Conduction Wireless Bluetooth 5.3 Headphones Sports Earphones HiFi Sound Quality Waterproof TWS Headset
Affliate products $3.33






