SOMA HII BALAAA NILIACHA CHUO KWA SABABU YA MAPENZI FAHAMU NINI KILICHO MKUTA DADA HUYU CLIK HERE……

Admin Updates10 years ago80 Views

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXw_OSRotJe3NlD85I-_0jQBSNWxeWuomyH1ugy5cKTnwUe7KgZDhy4mjq_CqsisqhxjbCo0jQeIodLqQCerRVm-EHl0ZP5SX0xX8nwBB-7j3Ah6-VsvXsdlKauJFFqyseNH7mIGN725w/s1600/P.jpgimi ni binti wa miaka 23, ninaishi na


wazazi wangu wote wawili, ni mtoto wa pili


kuzaliwa kwenye familia yetu. Nilianza


mahusiano ya kimapenzi nikiwa chuoni


mwaka wangu wa kwanza na kijana mmoja


aitwaye Erick, Nilitokea kumpenda sana


kwani alikuwa ndio mwanaume wangu wa


kwanza. Kwetu walimjua na hata kwao pia


nilifahamika.Nilikuwa na Erick mpaka


nilipofikamwaka wa pili hapo chuoni


Ambapo sasa tuliamua kukodi chumba


kimoja na kuishi wote. Katika kipindi hichi


niliona tabia za Erick hazieleweki anaweza


kurudi usiku sana akiwa hajitambui na hata


kulala tu chini mpaka asubuhi. Nilikuwa


nikimshauri lakini alikuwa ni mgumu sana


kunielewa.Siku moja alirudi akiwa mzima


majira ya saa kumi jioni hivi, kamasikosei


ilikuwa ni siku ya ijumaa, tena mimi nilikuwa


ndio natoka kwenye kipindi.Alikuja siku hiyo


akiwa na furaha sana huku akiwa na chupa


mbili moja ya wine na nyingine ya amarula,


Alizifungua zote nakuanza kunywa huku


tukipiga story na kucheka, na mimi


kwasababu pia nilikuwa nakunywa alini


miminia natukawatunakunywa wote, Nilipo


anza kulewa alianza kunishawishi nivute


sigara ambayo yeye alishaiwasha nakuanza


kuivuta bila kusita nilichukua sigara na


kuivuta kwakuwa nilimuamini sana


Erick.Muda si mrefu nilipata usingizi wa


ajabu ambao ulinifanya nisitambue


chochote kilichoendelea pale.Kesho yake


majira ya saa tano Asubuhi nilipata fahamu


na kuamka, nilimuuliza Erick kilichotokea


lakini hakunipa jibu lililo eleweka sikuwa na


raha kabisa kwani nilitamani kupata ileraha


tena, Nilishawishika kumuuliza erick kuhusu


ile sigara.na yeye hakunijibu ila alinipa tu


myingine akasema vuta hii hapa.Huu ndio


ulikuwa mwanzo wa kuharibu masomo


yangu. Kumbe kipindi chote Erick alikuwa


anatumia madawa ya kulevya akichanganya


kwenye sigara, na akaona haitosha anipe na


mimi.Basi na mimi niliendelea na tabia hiyo


hadi darasani nikawa siendi tena walimu


walikuwa wananiulizia sana kwani nilikuwa


kati ya wanafunzi wazuri sana darasani.


Niliendelea na tabia hiyo hadi wazazi wangu


walipokuja kujua na kunipeleka kwenye


kituo cha waathirika wa madawa. Kipindi


hicho Erick alikuwa amechanganyikiwa


kabisa kwa madawa na chuo alisha acha


yuko tu kwao.Nilikaa huko kwenye kituo


hicho kwa muda wa miezi sita, nikiwa


napata ushauri pamoja na dawa za


kupunguza hamu ya madawa ya kulevya.


Nashukuru sasa hivi niko nyumbani na


ninaendelea vizuri.

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko
Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...