
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu amewataka wageni wote wanaowasili mkoani humo kwa ajili ya Sikukuu za Christmas na Mwaka mpya kuhakikisha wanailinda amani ambayo wameikuta.
Babu ametoa kauli hiyo jana 10/12/2025 ofsini kwake mjini Moshi alipozungumza na Waandishi wa habari ambapo amesema kama ilivyo desturi ya mwisho wa Mwaka tayari sasa wameanza kupokea Wananchi wengi wenyeji wa Kilimanjaro wanaofanya shughuli zao nje ya mkoa huo na nchi mbalimbali ambapo kwa sasa kama ilivyozoeleka wanarejea kwa Wazazi wao na wengine kwenye makazi yao ya asili kwa ajili ya sikukuu za Mwisho wa Mwaka..
“Wengine wamerejea nyumbani kwa ajili ya kufanya mila za kufagia Makaburi huku wengine wamekuja kusalimia ndugu jamaa na marafiki” Alisema Babu.
Alitumia nafasi hiyo kuwakaribisha wageni wote anaoamini walitoka Kilimanjaro kwenda mikoa mingine kutafuta kwa njia za kujiajiri na wengine kufanya majukumu mbalimbali ya utumishi wa serikali ambapo pia ujio wao utachangia kuongeza mapato ndani ya Mkoa.
RC Rosemary Senyamue: Matokeo ya ziara ya Kidiplomasia ndani ya Jiji la Dodoma yameanza kuonekana






