MWARABU ALIYEKABIDHIWA SIMBA ANATISHA

7 years ago93 Views

Refarii wa Morocco
Kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya wenyeji Simba SC dhidi ya AS Vita, wachezaji wa Simba wanatakiwa kuwa na nidhamu ya hali ya juu, kutokana na mwamuzi wa mchezo huo Noureddine El Jaafari kusifika kwa kumwaga kadi na kutoa penati.

Noureddine El Jaafari raia wa Morocco, ameteuliwa na CAF kuchezesha mchezo huo wa Jumamosi kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam ambapo refa huyo ni mkali awapo kwenye majukumu yake.

Akiwa tayari ameshachezesha mechi kadhaa za hatua ya makundi msimu huu, Noureddine El Jaafari ameshatoa jumla ya kadi 18. Kati ya hizo kadi za njano ni 16 na kadi nyekundu ni 2.


Moja ya mechi ambayo Noureddine El Jaafari alichezesha na kutoa kadi nyingi ni ile ya kundi C kati ya CS Constantine dhidi ya TP Mazembe ambao ulimalizika kwa Mazembe kupoteza kwa mabao 3-0 huku yeye akitoa kadci 4 za njano ikiwa ni mbili kwa kila timu.

Wachezaji wa Simba ambao wamekuwa wakipata kadi za njano ni pamoja na Jonas Mkude, Juuko Murshid, Cletous Chama, Paul Bukaba pamoja na Emmanuel Okwi, hivyo wanatakiwa kuwa waangalifu zaidi katika mchezo huo.

from MALUNDE 1 BLOG https://ift.tt/2F1a85Y
via

0 Votes: 0 Upvotes, 0 Downvotes (0 Points)

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.