Mwananchi Aliyechoma Picha ya Rais Samia Akamatwa na Polisi Mbeya

1 year ago129 Views

 

Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya linamshikilia Shadrack Yusuph Chaula (24), mkazi wa Kijiji cha Ntokela kata ya Ndato wilayani Rungwe mkoani humo, baada ya kuchoma moto picha inayomuonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya SACP Benjamin Kuzaga, na kusema kuwa Juni 30 mwaka huu mtuhumiwa huyo ambaye ni msanii wa sanaa ya uchoraji alijirekodi video fupi akitamka maneno makali ya kumkashifu Rais Samia huku akichoma picha inayomuonesha Rais na kuisambaza mitandaoni.
Mapema leo asubuhi Julai 2, 2024, Mkuu wa mkoa wa Mbeya, alitoa saa 24 kwa Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani humo kuhakikisha kwamba kijana huyo anakamatwa kwani kitendo alichokifanya si cha kimaadili wala kiungwana na kiko tofauti na utamaduni halisi wa wakazi wa mkoa huo.

Join Us
  • Facebook38.5K
  • X Network32.1K
  • linkedin12.6k
  • youtube23.4k
  • Instagram18.9K
Mchanganyiko

Loading Next Post...
Follow
Sign In/Sign Up Search Trending 0 Cart
Popular Now
Loading

Signing-in 3 seconds...

Signing-up 3 seconds...

Cart
Cart updating

ShopYour cart is currently is empty. You could visit our shop and start shopping.