
MAMY BABY Ateuliwa kuwania Ubunge TABORA Aandika Haya Maneno mazito
Naishukuru sana Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya chama changu, Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa kuniteua na kunipendekeza kuwania Ubunge Viti Maalum (UWT) Mkoa wa Tabora. Niko tayari kutumika na kuwa Sauti Ya Tabora. CCM na Serikali yake imefanya mageuzi makubwa katika kujenga uchumi wa mtu mmoja mmoja na wa Mkoa wetu muhimu wa Tabora kwa ujumla.
Kwa nafasi hii na ridhaa nitakayoipata iwapo wanachama wenzangu watanipa nafasi hapo Julai 30, 2025 kwenye uchaguzi wetu wa Mkoa, nitatumia vipaji na vipawa vyangu, na kwa kushirikiana na viongozi wenzangu, kwa unyenyekevu na kujituma sana kuwainua akina mama na mkoa wetu kwa ujumla. Kwa wale wajumbe naomba kura yako, kwa Watanzania wenzangu wengine tuombeane kura na dua.
#SAUTIYATABORA
#MkuweAbdulIssale






