
LIVE: Chongolo na Makonda kwenye Uzinduzi wa Kampeni za CCM 2025
Wagombea Ubunge kwa Tiketi ya CCM Ndg Daniel Godfrey Chongolo (Makambako) na Paul Christian Makonda (Arusha Mjini) wakisalimiana kwa Furaha walipokutana Wiki iliyopita 28/08/2025 katika Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe Jijini Dar es Salaam zinakofanyika kampeni za Chama Caham mapinduzi (CCM) kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika kote nchini tarehe 29/10/2025 nchi nzima.

Mgombea Ubunge Jimbo la Makambako (CCM) Ndg.Daniel Chongolo na Mgombea Ubunge Jimbo la Arusha Mjini (CCM) Ndg.Paul Makonda wakifurahia jambo walipokutana kwenye Uzinduzi wa Kampeni za CCM Kitaifa zilizoongozwa na Mhe Dr Samia Suluhu Hassan ambaye Pia ndiye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na Mgombea Urais kwa Tiketi ya CCM akiambatana na Mgombea Mwenza Dkt.Emmanuel John Nchimbi,Viongozi wandamizi wa Chama pamoja na Wastaafu.

Ikumbukwe Ndg.Chongolo na Makonda wote waliwahi kuwa Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi kwa nyakati Tofauti Huku Chongolo Akihudumu kama Katibu Mkuu CCM na Makonda akihudumu kama Katibu wa Mafunzo itikadi na uenezi na sasa Wamekutana kama wagombea wa Ubunge kwenye majimbo yao.
SOMA HIZI HAPA:
RC Daniel Chongolo aipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Ileje kwa Kupata Hati Safi
BREAKING: Katibu Mwenezi CCM Taifa Kenani Kihongosi ameanza hiviiiii
Soma Magazeti ya Leo Alhamisi,28 Agosti 2025
Chongolo,Ridhiwani,Mavunde,Nanauka,Makonda na wengine Washinda kura za maoni






