
Akili mnemba ya jumla (kwa Kiingereza; Artificial General Intelligence au AGI kwa kifupi) ni tafiti za kinadharia ya akili mnemba inayojaribu kuunda programu ya kompyuta yenye utashi wa kibinadamu na zaidi, yenye uwezo wa kujifundisha yenyewe. Lengo la tafiti hii ni kuunda programu ya kompyuta yenye uwezo wa kufanya kazi ambazo haikufundishwa wala kuundwa kwa ajili ya kazi hizo.
Mifumo ya sasa ya akili bandia hufanya kazi chini ya mipaka iliyowekwa na waundaji wake, mfano, mfumo wa akili bandia wa kutambua au kuunda picha hauwezi kutengeneza wavuti.
Akili bandia ya jumla ni harakati ya kuunda mfumo wa akili bandia unaoweza kujiongoza, unaojitambua na wenye uwezo wa kujifunza ujuzi mpya. Wenye uwezo wa kutatua matatizo magumu katika mazingira na muktadha ambao haikufundishwa wakati wa uumbaji wake.
INGIA HAPA UJIFUNZE ZAIDI JINSI YA KUTUMIA AI TUMIA ===>> Masama Blog AI






