Mshindi wa shindano la Big Brother Africa 2014, Idris Sultan na msanii wa Bongo Fleva Ommy Dimpoz waliungana kwa kuhudhuria mahafali ya kidato cha nne ya Mbezi High School, Mbezi ya Kimara Dar es salaam.
Inawezekana unajua ama hujui mtu wangu lakini Idris Sultan na Ommy Dimpozwanashare kitu kimoja muhimu, mastaa hawa wawili walishawahi kusoma shule moja ambayo ndio hiyo Mbezi High School japo miaka tofauti ambapo kwenye mwaliko huu wa mahafali ya kidato cha nne alikuwemo pia Waziri wa habari, utamaduni na michezo, Dr. Fenella Ephraim Mukangara.
![IMG-20151017-WA0029[1]](http://i0.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/10/IMG-20151017-WA00291.jpg?resize=561%2C374)
Ommy Dimpoz, Idris Sultan na Dr. Fenella Mukangara kwenye picha ya pamoja na viongozi wengine wa shule ya Mbezi High School.